0
Ukosefu wa bajeti ya kutosha inayotengwa na serikali katika wizara ya mifugo na uvuvi ambayo ingewezesha kuandaa nyanda za malisho kwa wafugaji wa asili na matumizi bora ya ardhi  imetajwa kuwa ni chachu  ya kuendelea kwa migogoro kati ya wafugaji wakulima na wawekezaji inayo shamiri kwa kasi hapa nchi  kuongeza uhasama kwa makundi hayo na kughalimu uhai wa watu  wasiyo na hatia.
Kauli hiyo imesemwa na wadau wa sekta ya mifugo na wenyeviti wa halmashauri kutoka wilaya sita zinazo ongoza kwa migogoro ya ardhi kati ya  wafugaji  wakulima na wawekezaji zikiwemo wilaya za Mvomero,Kiteto,Kilindi,Bunda Serengeti na Simanjiro wanao kutana mkoani Singida kujadili mbinu za kupunguza migogoro inatokana na makundi hayo na upatikanaji wa nyanda za malisho na matumizi bora ya Ardhi.
 
Kwa upande wao wataalam wa kilimo na mifugo kutoka katika halmashauri hizo wamesema serikali imejitahidi kuchangia sekta hiyo kwa kupitia miradi ya PADEP na ASDP kauli ambayo imeonesha kuto kubalika na baadhi ya viongozi wa halmashauri waonalamikia ufinyu wa bajeti katika sekta hiyo inayo kabiliwa na migogoro kila kukicha.
 
Nawo watalam wa mifugo kutoka taasisi binafsi wamesema hayo yote yatawezekana endapo serikali itakuwa tayari kushirikiana na sekta binafsi na wadau wananguvu kubwa katika kuishiniza serikali.

Chapisha Maoni

 
Top