
Maafisa wa polisi nchini Kenya wameanzisha uchunguzi kuhusu picha zilizowekwa katika mitandao ya kijamii zinazoonyesha maafisa wa polisi wakiwachapa viboko raia wa Somalia.
Waathiriwa hao wametambulika kama raia wa Somalia ambao wamevuka na kuingia nchini Kenya kupitia eneo la kazkazini mashariki mwa Kenya.
Picha hizo zilichapishwa katika mtandao wa facebook wa afisa mmoja wa polisi kutoka eneo hilo.
Chapisha Maoni