Watu wawili wameripotiwa kujeruhiwa baada ya ndege moja ndogo kuanguka katika eneo la makazi la Chofu lililoko mjini Tokyo nchini Japan.
Ajali hiyo ilitokea nyakati za asubuhi ambapo nyumba tatu pamoja na magari mawili pia yaliteketea.
Timu ya wazima moto wanaarifiwa kuwasili katika eneo la tukio na kuanza shughuli za uokoaji.
Watu watatu wameripotiwa kuokolewa kutoka kwenye eneo la tukio huku wawili kati yao wakisemekana kuwa katika hali mbaya.
Ajali hiyo ilitokea katika eneo lililokuwa karibu na uwanja wa ndege wa Chofu ambao hutumika kwa ajili ya ndege ndogo nchini Japan.
DKT. CHARLES STEPHEN KIMEI ACHUKUA FOMU YA KUWANIA UBUNGE AWAMU YA PILI -
VUNJO
-
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mhe Dkt Charles Stephen Kimei amechukua
fomu ya kuwania ubunge awamu ya pili katika jimbo hilo zilizotolewa ofisi
za C...
Dakika 13 zilizopita
Chapisha Maoni