
WAZAZI wa
wanafunzi wanaosoma shule za msingi Mgongo na Kigonzile, Kata ya Nduli
manispaa ya Iringa wamempongeza Diwani wao, Bashir Mtove kwa kusimamia
ujenzi wa vyoo ambavyo vilikuwa vikitishia afya ya watoto wao.
Wakizungumza
na Uhuru, wazazi hao walisema kwa kipindi kirefu shule hizo zilikuwa
zikikabiliwa na uhaba mkubwa wa matundu ya vyoo jambo ambalo lingeweza
kusababisha magonjwa ya mliuko.
Walisema kuna wakati wanafunzi wa shule hizo walikuwa wakilazimika kuingia maporini kutokana na uhaba huo.
Mkazi wa
Kigonzile, Abibedi Kanywaga alisema tangu kuchaguliwa kwa diwani huyo
katika uchaguzi mdogo, uliofanyika mwaka mmoja uliopita, ujenzi wa vyoo
vya shule umeenda kwa kasi kutokana na usimamizi wa karibu.
Diwani wa
kata hiyo, Mtove alisema kutokana na tatizo kubwa la uhaba wa matundu
ya vyoo shuleni hapo aliamua kuita mkutano wa wazazi, na kuwashirikisha
namna gani watatatua changamoto hiyo.
Alisema
kwa kushirikiana na wananchi wake, walipata fedha kidogo toka kwa
wafadhili mbalimbali ikiwemo serikali, na kuamua kuunganisha nguvu zao
kuanza ujenzi wa vyoo hivyo.
Alifafanua
kuwa kwa muda mfupi ujenzi wa vyoo ulikamilika na kwamba, shule hizo ni
kati ya shule zenye vypoo bora kwa manispaa nzima ya Iringa kiasi
ambacho huzilazimu shule nyingine kwenda kujifunza.
Mbali na
ujenzi wa vyoo hivyo, Mtove alisema ameanza kushughulikia tatizo la
baadhi ya maeneo kukosa shule na hivyo kuwalazimu wanafunzi kutembea
umbali mrefu kwa ajili ya kufuata masomo.
Aliyataja
maeneo hayo kuwa ni Kipululu ambako wanafunzi hutembea umbali wa
kilometa 14, kufuata shule iliko na Msisima ambako wananchi wake
hutembea umbali wa kilometa 12.
Kutokana
na umbali huo alilazimika kuwashawishi, wazazi kujenda darasa moja
ambapo mwaka huu wanafunzi wa darasa la kwanza, wameanza kusoma kwenye
maeneo yao na kuwa ujenzi wa shule unaendelea.
Chapisha Maoni