Kauli hii ni msumari katika kidonda cha Morsi ambaye alikuwa tayari anatumikia kifungo cha miaka 20 jela kwa kuamrisha kukamatwa kwa waandamanaji waliopinga utawala wake.
Kufuatia uamuzi wa mahakam hiyo wa kunyongwa kwa Morsi , sasa kauli ya mwisho itapatikana tu baada ya uamuzi kutumwa kwa kadhi mkuu nchini humo ambaye ndiye atakayetoa uamuzi wa mwisho iwapo Morsi atanyonyongwa au la.
Hata hivyo Sheria za nchi hiyo bado zinamruhusu Morsi kukata rufaa licha ya uamuzi wa kadhi mkuu.
Morsi na wafuasi wake wamekuwa wakishikilia kukutu kuwa mashtaka dhidi yake yamechochewa na uhasama wa kisiasa baina yake na uongozi ulioko sasa.
Chapisha Maoni