0

KAMPUNI YA HUAWEI YAZINDUA NA SIMU MPYA YA KISASA YA P8

-Itaanza kuuzwa nchini wiki hii

Johannesburg, Julai 3: 2015:Shamrashamra za kila aina zilitawala jana mjini Johanesburg nchini Afrika ya Kusini wakati  kampuni ya Huawei ilipozindua simu mpya ya Smartphone ya kisasa aina ya P8 katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa klabu ya Country.

Mji wa Johannesburg ni moja ya miji mikubwa ya utalii duniani miji mingine ikiwa ni Bangkok,Singapore,Newyork na London ambako pia uzinduzi umefanyika ambapo Meneja Mpya wa Bidhaa za wateja na Biashara ukanda wa  Huawei Afrika ya Kusini Charlene Munillal   alizindua simu hii ya kisasa na kuonyesha jinsi ilivyotengenezwa kwa kiwango cha juu cha ubunifu kwa kukidhi matumizi ya aina mbalimbali katika soko.

Simu hii itakuwa kwenye soko la Afrika na nchi nyinginezo kuanzia katikati ya mwezi huu kwa Tanzania simu hii itaanza kupatikana katika soko la ndani ya muda wa wiki moja kuanzia sasa kwa bei ya gharama nafuu na wateja 100 watakao agiza simu hizi kupitia tovuti ya Huawei Tanzania kuanzia kesho watajishindia zawadi mbalimbali zenye thamani ya shilingi 300,000/-
"Lengo la  kuleta simu hii  ya Huawei P8  kwenye soko ni kuwawezesha wateja  wote duniani kupata simu ambayo ni  ya kisasa na rahisi kuitumia ikiwa inakidhi mahitaji mbalimbali na simu hii inathibitisha  dhmira ya kampuni yetu ya kuendelea kuingiza bidhaa bora za mawasiliano kwenye soko”Amesema Charlene Munillal Meneja Mkuu wa Huawei Afrika ya Kusini anayeshughulika na bidhaa na wateja.

Simu ya P8 yenye muundo wa kuvutia ambayo imetengenezwa kwa  kiwango cha juu cha kiteknolojia ambayo ni rahisi kwa mtu yeyote kuitumia ina mvuto wa pekee kwa watumiaji na itaanza kuingia kwenye soko la Afrika ya Kusini katika wiki ya pili ya mwezi huu.

Charlene anasema simu ya P8 imetengenezwa kwa kutumia malighafi bora ikiwa na ganda la nje lililotengenezwa kwa madini ya Alminium na inavutia kwa kila kwa mwonekano na ina uimara wa hli ya juu bila kusahau kiwango kikubwa cha kiteknolojia kinachomuwezesha mtumiaji kuitumia kwa matumizi ya aina mbalimbali.Ina urefu wa  mm6.4 na uzito wa gramu 144 na inapatikana katika rangi za aina mbalimbali kulingana na mahitaji ya mteja ambazo ni Shaba,Dhahabu,Nyeusi na kijivu.

Muundo wake kuanzia mwonekano,ubunifu wa kiteknolojia uliotumika kuitengeneza na urahisi wake kutumia kuweza kutumika kwa huduma za ziada kama vile kupiga picha na video bora ni moja ya mambo yanayoifanya simu hii kuwa  ya aina  yake na kuwa na sifa ya kipekee.

Programu ya Android Lollipop 5.0 inayopatikana katika simu hii mpya inarahisisha kuona,kutuma na kupokea ujumbe mfupi wa maneo hata wakati ambapo kioo cha simu kinakuwa kimezimwa na kuna programu ya kuhifadhi kumbumbu za mtumiaji zisisomwe na mtu asiyehusika nazo hata wakati ambapo simu inakuwa imepotea ama kuibiwa.Inazo programmu nyingi za kisasa ambazo zinarahisisha kutafuta taarifa mbalimbali kwa urahisi kwenye mtandao wa Google bila usumbufu wa aina yoyote.

Sifa nyingine ya pekee katika simu hii mpya ya P8 ni kuwa na uwezo wa kuongezeka sauti kuwa kubwa kwa kiwango cha asilimia 58 zaidi ya kiwango cha kawaida iwapo mtumiaji anakuwa kwenye sehemu zenye kelele na kuwa rahisi kwake kuendelea kupata mawasiliano na haina mawimbi endapo mtumiaji anaitumia kwa kutumia waya maalumu wa kusikilizia simu masikioni au unapotumia kipaza sauti kimoja cha simu bila kusahau kudumu na chaji ya betri kwa muda mrefu.

Pia simu hii mpya mbalina kuwa na mambo mengi ya kisasa na yanayoleta furaha kwa mtumiaji inaouwezo wa kuifadhi kiasi kikubwa cha kumbukumbu kufikia 16GB AU 64GB na ikiunganishwa na  interneti inakuwa na kasi ya ajabu katika kupakua data uwezo wake ukiwa zaidi ya mara tatu  ya uwezo wa simu zilizotengenezwa na makampuni mengine zilizopo kwenye masoko hivi sasa na inao uwezo wa kudaka mawasiliano na kusikika vizuri hata iwapo mtumiaji anasafiri kwa kutumia treni iendayo kasi kwa mwendo wa Kilometa 300 kwa saa.

Mwisho
Kuhusu  Kampuni ya Huawei
Huawei ni kampuni inayoongoza duniani kwa kuzalisha bidhaa za kurahisisha mawasiliano na teknolojia na inarahisisha maisha kupitia ubunifu wa bidhaa bora za teknolojia ya habari na mawasiliano kukidhi matakwa ya wateja wanaotumia simu na vifaa vingine vya mawasiliano.

Huawei imeajiri wafanyakazi wapatao 150,000 duniani kote ambao wanafanya kazi na makampuni ya mawasiliano ya simu,wafanyabiashara wanaouza bidhaa za  mawasiliano na wateja wanaotumia bidhaa hizo.Huduma,bidhaa na ubunifu wa teknokojia ya mawasiliano wa Huawei umesambaa katika nchi zaidi ya 170 duniani na inahudumia zaidi  ya moja ya tatu wa watu duniani.Ilianzishwa mwaka 1987 na ni kampuni binafsi ambayo hisa zake zinamilikiwa na wafanyakazi wake.

Chapisha Maoni

 
Top