Kwa mara ya kwanza, madaktari nchini Colombia wametumia mbinu ya kutoa uhai kwa Ovido Gonzalez aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi ya saratani ya koo.
Gonzalez mwenye umri wa miaka 79, alitolewa uhai
katika hospitali moja ya mji wa Pereira baada ya kuhangaishwa kwa muda
mrefu na maradhi hayo yasiyokuwa na tiba.
Mahakama kuu ya katiba nchini Colombia iliwahi kuidhinisha mbinu hiyo ya kutoa uhai mwaka 1997 ingawa haikupitishwa rasmi na kamati ya sheria.
Baadaye, mahakama kuu ikatoa ombi la kupitishwa kwa mbinu hiyo ambapo
wizara ya afya iliunga mkono matumizi yake kwa masharti maalum
yaliyobainishwa.
Gonzalez amekuwa mtu wa kwanza kutolewa uhai kisheria nchini Colombia ingawa mbinu hiyo inaarifiwa kutumika kwa muda mrefu kinyume na sheria.
Sherehe za siku ya Kiswahili duniani zafana nchini Algeria
-
BALOZI wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, amesema lugha ya
Kiswahili inaendelea kukua na kuenea duniani ambapo sasa inazungumzwa na
watu ...
Saa 2 zilizopita
Chapisha Maoni