Kwa mara ya kwanza, madaktari nchini Colombia wametumia mbinu ya kutoa uhai kwa Ovido Gonzalez aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi ya saratani ya koo.
Gonzalez mwenye umri wa miaka 79, alitolewa uhai
katika hospitali moja ya mji wa Pereira baada ya kuhangaishwa kwa muda
mrefu na maradhi hayo yasiyokuwa na tiba.
Mahakama kuu ya katiba nchini Colombia iliwahi kuidhinisha mbinu hiyo ya kutoa uhai mwaka 1997 ingawa haikupitishwa rasmi na kamati ya sheria.
Baadaye, mahakama kuu ikatoa ombi la kupitishwa kwa mbinu hiyo ambapo
wizara ya afya iliunga mkono matumizi yake kwa masharti maalum
yaliyobainishwa.
Gonzalez amekuwa mtu wa kwanza kutolewa uhai kisheria nchini Colombia ingawa mbinu hiyo inaarifiwa kutumika kwa muda mrefu kinyume na sheria.
Bilioni 75.4 Zatikisa Arusha DC, Wanafunzi 20,000 Kunufaika
-
Na Pamela Mollel, Arusha
Habari njema kwa wakazi wa Arusha! Halmashauri ya Wilaya ya Arusha
imependekeza bajeti ya shilingi bilioni 75.4 kwa mwaka wa fed...
Saa 12 zilizopita
Chapisha Maoni