0


Wanafunzi  wa  Chuo  Kikuu cha Iringa  wakiwa katika mgomo  leo kutokana na kutopata mkopo kwa wakati ambapo inapelekea kushindwa  kabisa  kuendesha maisha  yao  chuoni  hapo baada ya  serikali  kupitia  bodi ya  mikopo  kuwacheleweshea  pesa  zao.
Viongozi  wa  serikali ya wanafunzi wa Chuo  Kikuu cha Iringa  wakiwatuliza  wenzao  leo baada ya mgomo wa wanachuo wa chuo cha UoI kugoma wakishinikiza kupewa mikopo yao ili kuendesha maisha chuoni hapo.
Mkuu  wa chuo  kikuu ya Iringa Prof Joshua Madumulla akizungumza na wanafunzi hao baada ya kutokea mgomo chuoni hapo leo asubuhi.
Mmoja wa wanafunzi  wa chuo kikuu cha Iringa akitoa malalamiko yake dhidi ya  bodi ya mikopo kwa kaimu mkuu wa mkoa wa Iringa Bi Angeline Mabula leo kuhusu kucheleweshewa  mikopo yao.
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa Bi Mabula akizungumza na wanafunzi hao wakati wa mgomo wa wananchuo wa chuo cha Iringa leo
Ulinzi   ulikuwa ni wakutosha chuoni hapo


Chapisha Maoni

 
Top