0

WANAFUNZI wa vyuo vikuu vya UDOM, Mkoani Dodoma na kile cha DUCE jijini Dar es Salaam, waliamua kuacha masomo na kugoma kushinikiza bodi ya mikopo kulipa mikopo yao. Mgomo huo unakuja siku mbili tu baada ya wenzao wa UDSM kugoma kwa madai kama hayo na hatimaye siku iliyofuatia wakalipwa. Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alilazimika kumtuma naibu waziri wa Afya Steven Kebwe na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Chiku Galawa ili kutuliza "mzuka" wa wanafunzi ambapo baadhi yao walilia kwa uchunghu kama Eva Joseph, ambaye naibu waziri alilazimika kufanya kazi ya ziada kumtuliza na kumbebeleza. Pichani juu ni wanafunbzi hao wa UDOM, wakionyesha bango
Kebwe akimfariji Eva
Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Chiku Galawa akihutubia wanafunzi hao ambao walikuwa watulivu wakati wote wa mgomo

Chapisha Maoni

 
Top