0
 

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye Akizungumza na waandishi wa Habari leo ,jijini Dar es Salaam, kuhusiana na kubadilika kwa tarehe ya mkutano wao kufuatia kuingiliana na Mkutano wa Baraza la Wawakilishi.KAMATI kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) inatarajia kukutana Mei 23 mjini Dodoma na kujadili ajenda mbalimbali kuelekea uchaguzi mkuu .
 
Akizungumza na waandishi wa Habari leo ,jijini Dar es Salaam,Katibu wa Halmashauri Kuu Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye amesema kuwa kubadilika kwa siku ya mkutano imetokana na kuingiliana na Mkutano wa Baraza la Wawakilishi.

Nape amesema kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) kitafanyika Mei 22 ambapo ajenda mbalimbali zitatolewa ikiwa ni pamoja na maoni ya Ilani ya CCM 2015-2020 ambayo itawasilishwa na Kamati iliyoundwa kwa kazi hiyo.

Chapisha Maoni

 
Top