
Katibu wa
NEC Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye Akizungumza na waandishi wa Habari
leo ,jijini Dar es Salaam, kuhusiana na kubadilika kwa tarehe ya mkutano
wao kufuatia kuingiliana na Mkutano wa Baraza la Wawakilishi.KAMATI
kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) inatarajia kukutana Mei 23 mjini Dodoma
na kujadili ajenda mbalimbali kuelekea uchaguzi mkuu .
Akizungumza
na waandishi wa Habari leo ,jijini Dar es Salaam,Katibu wa Halmashauri
Kuu Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye amesema kuwa kubadilika kwa siku ya
mkutano imetokana na kuingiliana na Mkutano wa Baraza la Wawakilishi.
Nape
amesema kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) kitafanyika Mei 22 ambapo ajenda
mbalimbali zitatolewa ikiwa ni pamoja na maoni ya Ilani ya CCM
2015-2020 ambayo itawasilishwa na Kamati iliyoundwa kwa kazi hiyo.
Chapisha Maoni