Wakizunguzia hatua ya kuibuka upya kwa mgogoro huo watetezi wa haki
za wafugaji kutoka mashirika yanayo jihusha na utetezi wamesema
kimsingi waziri mkuu Mizengo Pinda alishamaliza mgogoro huo mwaka jana
alipotembelea eneo ilo na kuruhusu shughuli za kifugaji kuendelea
sambamba na uhifadhi lakini hali imeanza kubadilika na kutishiwa maisha
kinyume na maamuzi ya waziri mkuu.
Mratibu wa mtandao wa wafugaji Tanzania Joseph Parsambey amesema
hatua hiyo ina lengo la kuwaumiza zaidi ya wakazi elfu themanini wanao
ishi katika vijiji nane vinavyo zunguka pori la akiba la Loliondo kwa
mgongo wa mapito ya wanyamapori huku lengo likiwa ni kuwapati wawekezaji
kutoka nje ya nchi na kuwa acha watanzania bila matumaini huku wanawake
nao wakilalamikia kuteseka kwa matukio yanayo jirudia na kuitaka
serikali iwe na msimamo kwani wanawake wa Loliondo kamwe hawataondoka
katika ardhi yao.
Mnamo tarehe ishirini na tatu mwezi wa tisa mwaka jana (2013)
waziri mkuu Mhe Mizengo Pinda alifanya ziara katika eneo lenye mgogoro
kutembelea vijiji vyote na kutoa maamuzi ya serikali kuwa imeamua wakazi
hao waendelee kuishi kama ilivyokuwa mwanzo maamuzi ambayo yanatajwa
kukiokwa bila taarifa kwa wananchi amba sasa wanatakiwa kuondoka katika
eneo ilo.
Chapisha Maoni