0

Afrika Kusini imeanzisha operesheni ya kuwafurisha raia zaidi ya 400 kutoka Msumbiji  kurudi makwao kufuatia vurumai ya kibaguzi dhidi ya wageni katika miji ya Durban na Johannesburg baada ya wenyeji kuanza  kuwavamia wageni pamoja na kuwapora mali zao jambo lililopelekea watu saba raia wa kigeni kuuawa na wenyeji waliokuwa wakilalama kuwa wageni hao wamechukua nafasi zao za kazi.
Serikali ya Msumbiji imeshangazwa na hatua hiyo ya kuwaondoa raia wake kwa nguvu huku waziri wake wa maswala ya kigeni Oldemiro Baloi akisema alikuwa anatarajia kufanya mazungumzo na mwenzake wa Afrika Kusini Baloi huyo ameongeza kuwa haelewi kwa nini raia wa Msumbiji wanakamatwa na kuondolewa nchini humo kwa nguvu ilihali swala hilo lilikuwa linashughulikiwa baina ya serikali hizo mbili.
 
BBC imesema hatua hii ya serikali imewashangaza wengi hususan baada ya serikali kupewa ilani ya mahakama dhidi ya kuwakamata na kuwafukuza wageni. ambapo ''Operesheni Fiela'' ya kuwakamata wageni imekuwa ikiendeshwa majira ya alfajiri hasa katika mitaa duni ya miji ya Durban na Johannesburg.
 
''Operesheni Fiela'' kama inavyofahamika imepelekea watu zaidi ya 889 kukamatwa na Wanaharakati wa haki za kibinadamu wamekwenda mahakamani kupinga operesheni Fiela wakisema inahalalisha vita vya kibaguzi vilivyo sababisha vifo vya watu saba wengi wao wakiwa raia wa mataifa ya Afrika.CHANZO:BBC (Muro)

Chapisha Maoni

 
Top