‘’AFRIKA INAPASWA KUHUSIKA NA UKUZAJI WA RASILIMALI ZAKE"
Zuma alisema, ‘’Tumekubaliana kama viongozi kwamba hatutoruhusu raslimali zetu za madini tunazozimiliki kukuzwa nje ya bara la Afrika. Shughuli zote za utengenezaji na ukuzaji zinapaswa kufanyika ndani ya Afrika ili kuweza kuwafaidisha watu wetu wa Afrika.’’
Wakati huo huo, Zuma pia alishiriki mashindano ya AU Presidential Golf Challenge yaliyolenga kuchangisha fedha kwa ajili ya miradi ya AU.
Zuma alitoa shukrani kubwa kwa wajumbe waliohudhuria mkutano wa AU na kudhihirisha furaha yake aliyokuwa nayo kwa kupata fursa ya kuandaa mkutano huo muhimu nchini Afrika Kusini. CHANZO TRT SWAHILI
Chapisha Maoni