Ikiwa mihula miwili ya rais Barack Obama ikielekea ukingoni, Ben Carson
ambae ni daktari mstaafu wa tiba ya mishipa amejitangaza kuwa atawania
kiti cha urais katika uchaguzi utakaofanyika nchini Marekani ifikapo
mwaka 2016.
Ben Carson ni mzawa wa jimbo la Detroit, jimbo ambalo linapatikna kaskazini magharibi mwa Marekani, alihitimu katika chuo kikuu cha Ivy League Yale na chuo kikuu cha Michigan.
Ben Carson ana umri wa miaka 64.
Daktari mtaalamu wa tiba ya mishipa, Ben Carson aliongoza kundi la madaktari 70 waliofaulu kuwaachanisha mapacha waliozaliwa wameshikana vichwa.
Ben Carson alikiambia kituo cha televisheni cha Fox News kuwa iwapo atachaguliwa, kodi itakuwa ikitolewa kwa misingi ya biblia "fungu la 10".
Baada ya mihula miwili ya Barack Obama, Ben Carson atachaguliwa kuwa rais wa 45 wa Marekani ?
CHANZO TRT SWAHILI
ZAIDI YA SHILINGI MILIONI MIA MOJA ZAKUSANYWA UJENZI WA OFISI YA CCM WILAYA
YA TUNDURU
-
Zaidi ya Shilingi milioni mia moja na mchango wa vifaa vya ujenzi, ikiwemo
saruji zimepatikana katika harambee ya uchangiaji wa ujenzi wa ofisi mpya
ya kis...
Dakika 58 zilizopita
Chapisha Maoni