Chama tawala cha Ethiopia EPRDF pamoja na washirika wake, kimeshinda viti 546 kati ya 547 bungeni kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 24 mwezi Mei mwaka huu.
Tume ya uchaguzi nchini Ethiopia NEBE, ilitangaza matokeo ya mwisho ya uchaguzi huo siku ya Jumatatu ambapo chama tawala kilitangazwa kushinda viti 500 vya bunge.
Viti vingine 46 vya bunge vilishindwa na wanasiasa wanaokiunga mkono chama tawala cha EPRDF
ikiwa 24 ni kutoka chama cha SPDP, 9 kutoka chama cha BGPDP, 8 kutoka
chama cha ANDP, 3 kutoka chama cha GPUDM, 1 kutoka chama cha HNL na
kingine 1 kutoka chama cha APDO.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa NEBE Merga Bekana, kiti kimoja cha bunge kilichobakia bado hakijabainishwa mshindi wake.
Kulingana na takwimu za NEBE, asilimia 93.2 ya wananchi milioni 36.8 waliojisajili, ndio waliojitokeza kupiga kura siku ya uchaguzi.TRT SWAHILI
IAA KUBORESHA MAZINGIRA YA KUJIFUNZIA ILI KUENDELEA KUZALISHA WATAALAM
MAHIRI
-
Na Mwandishi Wetu
MKUU wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka amesema IAA
itaendelea kuimarisha miundombinu na mazingira ya kujifunz...
Saa 15 zilizopita
Chapisha Maoni