Mama na mtoto wanusurika kimiujiza katika ajali ya ndege iliotokea nchini Colombia.
Mama na mtoto huyo walipatikana siku 5 baada ya ya ndege waliokuemo kupata ajali.
Rubani wa ndege hiyo aliripotiwa kufariki katika ajali hiyo.
Kikosi cha uokozi kilimuona mama huyo walipokaribia mabaki ya ndege hiyo.
Kabla ya kusitisha shuhuli yakuwatafuta wahanga wa ajali hiyo, mama na mtoto wake walibahatika kuokotwa na kikosi cha waokoaji.
Waokoaji hao walifahamisha kuwa mama huyo ambae alitambulika kwa jina la Nelly Murillo alijeruhiwa kidogo huku mwanawe Yudier Moreno akiwa salama.
Yudier Moreno akiwa na umri wa chini ya mwaka mmoja.
Nelly Murillo na Yudier walikuwa wasafiri pekee katika ndege ndogo ya uchukuzi Cessna 303 ambayo ilikuwa ikielekea Quibdo nchini Colombia.
JESHI LA POLISI LAPONGEZWA KWA KUIMARISHA ULINZI KARIAKOO
-
Na Mwandishi wetu ,Dar es salaam
KUTOKANA na uvunjifu wa amani na uharibifu wa miundombinu uliojitokeza kwa
siku nne hadi tano zilizopita kwa baadhi y...
Saa 8 zilizopita
Chapisha Maoni