Patrick Njoroge,amechaguliwa rasmi na rais kuwa gavana mpya Benki kuu ya Kenya baada ya bunge kupitisha uchaguzi huo.
Rais Uhuru Kenyatta, amemchagua Yairo Mohammed Nyaoga, kuwa mwenyekiti wa bodi ya benki hiyo na Sheila M'Mbijjewe kuwa naibu mkuu wa pili wa gavana.
Uteuzi huo umemaanisha kuwa mkutano wa kamati ya sera na shirika la fedha, unaotarajiwa kufanyika Julai 7 utafanywa na gavana mpya wa Benki kuu.
Haron Sirima, mmoja wa naibu magavana wa benki hiyo,aliyeendesha mkutano wa mwisho uliofanyika Juni 9. TRT SWAHILI
Bilioni 75.4 Zatikisa Arusha DC, Wanafunzi 20,000 Kunufaika
-
Na Pamela Mollel, Arusha
Habari njema kwa wakazi wa Arusha! Halmashauri ya Wilaya ya Arusha
imependekeza bajeti ya shilingi bilioni 75.4 kwa mwaka wa fed...
Saa 10 zilizopita
Chapisha Maoni