Kaimu
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Taaluma, Profesa George
Shumbusho (kulia) akiwasilisha mada wakati wa kongamano la majadiliano
ya rasimu ya mtaala wa Chuo Kikuu Mzumbe, Skuli ya Biashara, hivi
mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kongamano hilo lilihusisha wadau
mbalimbali kutoka sekta ya umma na binafsi.
Kaimu
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Taaluma, Profesa George
Shumbusho (kulia) akijadiliana jambo na Mkuu wa Skuli ya Biashara ya
chuo hicho, Dr. Hawa Tundui (kushoto) wakati wa kongamano la majadiliano
ya rasimu ya mtaala wa Skuli hiyo ya Biashara mwishoni mwa wiki jijini
Dar es Salaam. Kongamano hilo lilihusisha wadau mbalimbali kutoka sekta
ya umma na binafsi.
Chuo
Kikuu Mzumbe kimeanza rasmi awamu ya pili ya mchakato wa kuhuisha mtaala
unaotumika katika Skuli yake ya Biashara ili kuendana na hali hasi ya
mabadiliko yanayotokea haraka nchini na duniani katika nyanja za siasa,
uchumi, jamii na teknolojia.
Inatarajiwa
kuwa mabadiliko hayo yatasaidia pia kuwajengea zaidi uwezo wahitimu wa
chuo hicho kujiajiri na kuajiriwa kwa urahisi zaidi.
Kaimu
Naibu Makamu mkuu wa Chuo hicho, Taaluma, Profesa George Shumbusho
aliwaambia waandishi wa habari mwishoni mwa wiki mjini hapa kuwa
mabadiliko hayo yanalenga kutoa wahitimu watakaokuwa na uwezo wa
kushindana kitaifa na kimataifa katika nyanja za biashara, manunuzi, na
ujasiriamali.
Uongozi
na wataalamu wa chuo hicho ulikutana na wadau mbalimbali kutoka sekta ya
umma na binafsi kupitia rasimu ya mapendekezo ya mabadiliko ya mtaala
wa skuli ya chuo hicho.
“Ni utaratibu wa chuo chetu kuhakikisha kuwa tunapitia mitaala kila baada ya miaka mitatu ili kuihuisha,”alisema Prof. Shumbusho.
“Ni utaratibu wa chuo chetu kuhakikisha kuwa tunapitia mitaala kila baada ya miaka mitatu ili kuihuisha,”alisema Prof. Shumbusho.
Alisema
mwanzo skuli hiyo iliwaomba wadau wa chuo wakiwemo waajiri, wazazi na
taasisi mbalimbali kutoa mawazo yao kuhusu hitaji la kuwa na mtaala mpya
unaoendana na mabadiliko yanayojitokeza hapa nchini na ulimwengu kwa
ujumla.
Maoni
hayo yalichukuliwa na kuingizwa katika rasimu ya mtaala iliyopendekezwa
na kupitiwa na walimu na wanafunzi ambao waliandaa rasimu ya pili ambayo
ndio ilikuwa inajadiliwa tena na wadau hao.
Profesa
Shumbusho alisema baada ya kupata maoni ya wadau hao tena, watatoa
rasimu ya mwisho ambayo itajadiliwa na seneti ya chuo hicho na kupelekwa
Tume ya Vyuo vikuu (TCU).
Inatarajiwa kuwa mtaala huo utaanza kutumika mwezi Octoba 2015.
Mkuu wa Skuli ya Biashara, Dkt. Hawa Tundui alisema skuli hiyo imedhamiria kutoa elimu iliyo bora na kuwa shindani hapa nchini na katika eneo hili la Afrika.
“Tunataka kuleta manufaa zaidi kwa wahitimu, jamii, na nchi kwa ujumla,” alisema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Dkt. Clemence Tesha alisema mitaala ni lazima iendane na mageuzi yanayojitokeza la sivyo vyuo vitakuwa vinafundisha vitu vilivyopitwa na wakati.
Mkuu wa Skuli ya Biashara, Dkt. Hawa Tundui alisema skuli hiyo imedhamiria kutoa elimu iliyo bora na kuwa shindani hapa nchini na katika eneo hili la Afrika.
“Tunataka kuleta manufaa zaidi kwa wahitimu, jamii, na nchi kwa ujumla,” alisema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Dkt. Clemence Tesha alisema mitaala ni lazima iendane na mageuzi yanayojitokeza la sivyo vyuo vitakuwa vinafundisha vitu vilivyopitwa na wakati.
“Katika vyuo hili ni jambo la lazima ili kuiwezesha nchi kuwa na wasomi wanaoendana na wakati,”alisema.
Alisema
wao kama wadau wametoa maoni yao kwa mambo ya msingi yanayohitajika
kufanyika ili taifa liweze kuwenda sambambana na mahitaji ya soko na
nchi.
Baadhi ya
wadau walioshiriki katika kujadili rasimu hiyo ni pamoja na Wizara ya
Maji, Ofisi ya Waziri Mkuu, Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu
Tanzania (NBAA), PSPTB, Mamlaka ya Manunuzi nchini (PPRA), Mamlaka ya
Usimamzi na Udhibiti wa Huduma za Usafiri wa Majini na Nchi Kavu
(SUMATRA), benki ya CRDB, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, Kampuni za
Ukaguzi, na wajasilimali mbalimbali.(Muro)
Chapisha Maoni