Maafisa wa hospital wametaarifu kuwa takriban watu 64 wamefariki kufuatia joto kali kwa muda wa masaa 24 na idadi kuongezeka kufikia 84 kwa muda wa siku mbili nchini Pakistan.
Baadhi ya watu 15 wamefariki kufatia joto kali katika mji wa Karachi ambapo kiasi cha joto kufikia nyuzi joto 41.
Watu wengine 10 wamefariki katika mji wa Sibbi, Tharparkar na Shekhupur siku ya Jumamosi.
Daktari Seemi Jamali wa hospitali ya Jinnah aliiambia shirika la
habari la Anadolu "wagonjwa 30 waliletwa hosptali wakiwa na hali mbaya
na wengine 15 wamefariki dunia ikiwa wengıne 15 wameanza matibabu katika
mji wa Karachi."
Taarifa zinafahamisha kuwa zaidi ya watu 140 wamekwishafariki kutokana na joto hilo kali.
İdara ya hali ya hewa imetabiri kuendelea kwa joto kali kwa muda wa siku chache zijazo katika maeneo mengi ya nchi.
Hali hii itapelekea kukatika kwa umeme na kufanya mwezi wa Ramadhani kuwa mgumu.
YAS FIBER KUWEKEZA SHILINGI BILIONI 300 KUPANUA MKONGA WA MAWASILIANO
ZANZIBAR KWA KUSHIRIKIANA NA ZICTIA
-
Na Mwandishi Wetu Zanzibar
YAS Fiber Tanzania itawekeza takriban shilingi bilioni 300 kwa kipindi cha
miaka 20 ili kupanua huduma za intaneti yenye kasi...
Saa 14 zilizopita
Chapisha Maoni