0
Mgombea Ugavana wa Jimbo la Kisumu amewaahidi wapiga kuwa kuwa ataweka mazingira rafiki kwa wanaofanya biashara ya kuuza miili yao (makahaba) na kuhakikisha wanapata faida endapo watamchagua katika uchaguzi mkuu ujao.
 
Dkt. Hezron Mc’Obewa, ambaye anarusha karata yake ya ugavana katika jimbo hilo kumng’oa kiongozi aliyepo sasa, Jack Ranguma aliyasema hayo siku ya Jumanne alipokuatana na makahaba zaidi 300 katika Taasisi ya Goan.
 
Dkt. Mc’Obewa alisema kuwa atashinikiza mikutano ya kimataifa iwe inafanyikia pia Kisumu ili makahaba hao waweze kupata soko.
“Watu hawa hulipa vizuri wanapokwenda nchi za ugenini, na wafanyabiashara hao hupata hadi Ksh 200,000 kwa usiku mmoja” alisema mgombea huyo. “Mikutano hii mikubwa ndiyo huleta wateja watakaowalipa ninyi kwa viwango vywa kimataifa” aliongeza.
Mbali na ahadi hiyo iliyozua gumzo maeneo mengi, mgombea huyo amewaahidi kuwa atahakikisha kunakuwapo ajira za kutosha ili watu wawe na fedha kwenye mifuko yako.
 
“Biashara yenu ninyi itakuwa na faida kama wanaume watakuwa na fedha mfukoni, na hii ndio sababu lazima tuhakikishe tunamaliza ukosefu wa ajira” alisema Dkt. Mc’Obewa.
Mgombea huyo alisema kiongozi wa sasa wa jimbo hilo hawajali kabisa makahaba hao ambao chini ya mwamvuli wa Kisumu Sex Workers Sacco. Hivyo amewasihi kumchagua yeye ili waweze kufurahia biashara yao na atahakikisha anaimarisha ulinzi dhidi yao.
 
“Wakati mwingine unapata mteja ambaye anakupakiza kwenye gari lake, lakini usalama wako unakuwa ni mdogo, au unafayia kazi katika mazingira machafu ambayo yanahatarisha afya yako. Haya yote ndiyo tunataka yabadilike”, alisema.Aidha, mgombea huyo aliwataka makahaba hao kujisajili katika Shirika la Taifa la Bima ya Afya (NHIF) ili kuweza kupata huduma za kitabibu.

Chapisha Maoni

 
Top