
Akimkaribisha mgeni rasmi kaimu mkuu wa wilaya ya Mbongwe ambaye
pia ni mkuu wa wilaya ya bukombe Amani Mwenegoha amewataka wananchi
kuacha kukimbilia kwa waganga wa kienyeji kupata tiba ya Fistula na
badala yake wawapeleke hospitali ili kupatiwa tiba sahihi.
Naye msanii maarufu nchini Mrisho Mpoto amesema iko dhana potofu ya
kuwa mwanamke anayeugua fistula alikuwa na wanaume wengi kipindi cha
ujauzito jambo ambalo si kweli hata kidogo.
Awali akizungumza katika uzinduzi wa kampeni ya kutokomeza ugonjwa
wa fistula kwa akina mama waliopata uzazi pingamizi Naibu waziri
tamisemi katika ofisi ya waziri mkuu Kassimu Majaliwa amesema vita ya
kupambana na ugonjwa wa fistula ni ya kila mtu hivyo kuwataka wananchi
kutoa ushirikiano pale watakapomuona mgonjwa.
Kampeni ya kutokomeza ugonjwa wa Fistula inafanywa na mashirika
yasiyo ya kiserikali kama hospitali ya
CCBRT,VODACOMFOUNDATION,UNFP,AMREF ambapo mikoa mitano itatembelewa na
kupata elimu hiyo kwa awamu ya kwanza.
Chapisha Maoni