Mwili wa aliyekuwa kiongozi wa karibu wa Saddam Husein Tareq Aziz, umewasili katika mji mkuu wa Amman nchini Jordan.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa familia na baadhi vyanzo vya habari, jeneza la Tareq Aziz lilidaiwa kutoroshwa na kundi moja la watu waliojihami kwa silaha.
Serikali ya Iraq imekanusha madai hayo na kusema kwamba jeneza hilo lilisubirishwa Baghdad kwa muda kutokana na baadhi ya taratibu zilizokuwa zikifuatiliwa.
Waziri Mkuu wa Iraq Haydar Abadi, alitoa idhini ya kuwasilishwa kwa jeneza la Tareq Aziz kwa familia yake nchini Jordan pasi na kufanyiwa sherehe wala maandamano ya aina yoyote.
Tareq Aziz ambaye ni waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Iraq
na aliyewahi kuhudumu kama naibu waziri mkuu wakati wa utawala wa
Saddam Husein, alifikishwa hospitalini kutoka kwenye gereza alilofungwa
na kupoteza maisha tarehe 5 mwezi Juni akiwa na umri wa miaka 79. CHANZO: TRT SWAHILI
Bilioni 75.4 Zatikisa Arusha DC, Wanafunzi 20,000 Kunufaika
-
Na Pamela Mollel, Arusha
Habari njema kwa wakazi wa Arusha! Halmashauri ya Wilaya ya Arusha
imependekeza bajeti ya shilingi bilioni 75.4 kwa mwaka wa fed...
Saa 12 zilizopita
Chapisha Maoni