Mjumbe mmoja wa Umoja wa Afrika (AU) kutoka Nigeria, ameripotiwa kuporwa na watu waliovalia mavazi ya polisi katika mji wa Johannesberg nchini Afrika Kusini.
Mjumbe huyo kwa jina la Gabriel Gundo, alikumbwa na
mkasa huo alipokuwa akisafiri kutoka uwanja wa ndege wa OR Tambo
kuelekea Sandton ili kuhudhuria mkutano wa AU.
Gundo mwenye umri wa miaka 55, alisimamishwa na waporaji
waliovalia mavazi ya polisi na kuporwa fedha dola 500 za Kimarekani
alizokuwa amebeba pamoja na noti kadhaa za fedha za ndani ya nchi.
Msemaji wa idara ya polisi amearifu kwamba uchunguzi unaendelea kufanyika kuhusiana na tukio hilo.CHANZO TRT SWAHILI
Bilioni 75.4 Zatikisa Arusha DC, Wanafunzi 20,000 Kunufaika
-
Na Pamela Mollel, Arusha
Habari njema kwa wakazi wa Arusha! Halmashauri ya Wilaya ya Arusha
imependekeza bajeti ya shilingi bilioni 75.4 kwa mwaka wa fed...
Saa 12 zilizopita
Chapisha Maoni