Kituo cha polisi cha Afrika Kusini kimedai kutafuta kibali cha kukamatwa kwa Rais wa Sudan Omar al-Bashir, kama atahudhuria mkutano utakofanyika katika mji wa Santon nchini Afrika kusini.
Mkurugenzi wa shirika lenye makao makuu yake mjini Johannesburg Kaajal Ramjathan-Keogh,
alinukuliwa na vyombo vya habari nchini akisema kuwa alikuwa amepokea
taarifa ya kutafutwa na Mahakama ya kimataifa rais wa Sudani al-Bashir.
Rais al-Bashir, amekuwa rais wa kwanza katika orodha ya marais
wanaotafutwa na mahakama ya kimataifa baada ya kesi kusikilizwa na
kutolewa kibali cha kukamatwa.
Al-Bashir, anashukiwa kwa makosa matano ya uhalifu dhidi ya ubinadamu
(mauaji, kuteketeza kizazi, uhamishaji kwa kutumia nguvu, mateso ya
ubakaji).
Na pia anashukiwa makosa mengine mawili ya uhalifu wa kivita
(mashambulio ya moja kwa moja dhidi ya raia) katika jimbo la Darfur
nchini Sudan.CHANZO TRT SWAHILI
Bilioni 75.4 Zatikisa Arusha DC, Wanafunzi 20,000 Kunufaika
-
Na Pamela Mollel, Arusha
Habari njema kwa wakazi wa Arusha! Halmashauri ya Wilaya ya Arusha
imependekeza bajeti ya shilingi bilioni 75.4 kwa mwaka wa fed...
Saa 10 zilizopita
Chapisha Maoni