Kituo cha polisi cha Afrika Kusini kimedai kutafuta kibali cha kukamatwa kwa Rais wa Sudan Omar al-Bashir, kama atahudhuria mkutano utakofanyika katika mji wa Santon nchini Afrika kusini.
Mkurugenzi wa shirika lenye makao makuu yake mjini Johannesburg Kaajal Ramjathan-Keogh,
alinukuliwa na vyombo vya habari nchini akisema kuwa alikuwa amepokea
taarifa ya kutafutwa na Mahakama ya kimataifa rais wa Sudani al-Bashir.
Rais al-Bashir, amekuwa rais wa kwanza katika orodha ya marais
wanaotafutwa na mahakama ya kimataifa baada ya kesi kusikilizwa na
kutolewa kibali cha kukamatwa.
Al-Bashir, anashukiwa kwa makosa matano ya uhalifu dhidi ya ubinadamu
(mauaji, kuteketeza kizazi, uhamishaji kwa kutumia nguvu, mateso ya
ubakaji).
Na pia anashukiwa makosa mengine mawili ya uhalifu wa kivita
(mashambulio ya moja kwa moja dhidi ya raia) katika jimbo la Darfur
nchini Sudan.CHANZO TRT SWAHILI
DKT. MWIGULU AZUNGUMZA NA WANANCHI WALIOATHIRIWA NA MVUA KILOSA.
-
*Autaja mradi wa ujenzi wa mabwawa ya kuhifadhi maji ya Mvua eneo la Kidete.
WAZIRI Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amezungumza na wakaz...
Dakika 30 zilizopita
Chapisha Maoni