Hukumu iliyotolewa ya kumfungia mechi nne nyota wa Barcelona na nahodha wa timu ya taifa ya Brazil, Neymar Jr imemsababishia nyota huyo kutoshiriki mchezo wowote uliosalia katika Copa America.
Neymar alipata adhabu hiyo baada ya kumpiga na mpira mchezaji wa Colombia ambapo katika mechi hiyo Brazil ililala kwa goli moja kwa nunge.
Brazil ilitinga uwanjani Jumapili kukipiga na Venezuela na kuweza kuibuka na ushindi wa magoli 2 kwa moja.
Nyota wa Barcelona na mshindi mara nne wa tuzo ya Ballon d’Or, Lionel Messi alielezea kusikitishwa kwake na hukumu hiyo iliyompata Neymar.
Messi alisema kuwa Neymar ni mchezaji muhim kwa Brazil na Brazil imepata pengo.
JESHI LA POLISI LAPONGEZWA KWA KUIMARISHA ULINZI KARIAKOO
-
Na Mwandishi wetu ,Dar es salaam
KUTOKANA na uvunjifu wa amani na uharibifu wa miundombinu uliojitokeza kwa
siku nne hadi tano zilizopita kwa baadhi y...
Saa 8 zilizopita
Chapisha Maoni