Hukumu iliyotolewa ya kumfungia mechi nne nyota wa Barcelona na nahodha wa timu ya taifa ya Brazil, Neymar Jr imemsababishia nyota huyo kutoshiriki mchezo wowote uliosalia katika Copa America.
Neymar alipata adhabu hiyo baada ya kumpiga na mpira mchezaji wa Colombia ambapo katika mechi hiyo Brazil ililala kwa goli moja kwa nunge.
Brazil ilitinga uwanjani Jumapili kukipiga na Venezuela na kuweza kuibuka na ushindi wa magoli 2 kwa moja.
Nyota wa Barcelona na mshindi mara nne wa tuzo ya Ballon d’Or, Lionel Messi alielezea kusikitishwa kwake na hukumu hiyo iliyompata Neymar.
Messi alisema kuwa Neymar ni mchezaji muhim kwa Brazil na Brazil imepata pengo.
YAS FIBER KUWEKEZA SHILINGI BILIONI 300 KUPANUA MKONGA WA MAWASILIANO
ZANZIBAR KWA KUSHIRIKIANA NA ZICTIA
-
Na Mwandishi Wetu Zanzibar
YAS Fiber Tanzania itawekeza takriban shilingi bilioni 300 kwa kipindi cha
miaka 20 ili kupanua huduma za intaneti yenye kasi...
Saa 14 zilizopita
Chapisha Maoni