Rais wa Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila ametoa wito wa mazungumzo baina ya wakongomani wenyewe bila kuingiliwa kati.
Wito huo umetolewa baada ya upinzani kuomba mazungumzo na wawakilishi wa kimataifa.
Katika sherehe za kuazimisha maika 55 ya uhuru wa Jamuhuri ya Kidemokrasia, rais Kabila alifahamisha kuwa alitilia maanani ombi la upinzani kuhitaji mazungumzo na serikali.
Rais Kabila alifahamisha kuwa yupo tayari kwa mazungumzo ila bila ushirikiano wa kimataifa.
Upinzani nchini humo ulifahamisha kuwa katika mazungumzo hayo ni muhimu kuepo na wawakilishi wakimataifa.TRT SWAHILI
MENEJA TRA WILAYA YA BAHI ASISITIZA USAJILI WA TIN NA MALIPO YA KODI AWAMU
YA TATU
-
Na. Yahya Saleh-Bahi
Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma Bw.
Emmanuel Nyeme amewataka Wafanyabiashara na Walipakodi...
Dakika 44 zilizopita
Chapisha Maoni