Watu wawili wameripotiwa kujeruhiwa baada ya ndege moja ndogo kuanguka katika eneo la makazi la Chofu lililoko mjini Tokyo nchini Japan.
Ajali hiyo ilitokea nyakati za asubuhi ambapo nyumba tatu pamoja na magari mawili pia yaliteketea.
Timu ya wazima moto wanaarifiwa kuwasili katika eneo la tukio na kuanza shughuli za uokoaji.
Watu watatu wameripotiwa kuokolewa kutoka kwenye eneo la tukio huku wawili kati yao wakisemekana kuwa katika hali mbaya.
Ajali hiyo ilitokea katika eneo lililokuwa karibu na uwanja wa ndege wa Chofu ambao hutumika kwa ajili ya ndege ndogo nchini Japan.
Bilioni 75.4 Zatikisa Arusha DC, Wanafunzi 20,000 Kunufaika
-
Na Pamela Mollel, Arusha
Habari njema kwa wakazi wa Arusha! Halmashauri ya Wilaya ya Arusha
imependekeza bajeti ya shilingi bilioni 75.4 kwa mwaka wa fed...
Saa 10 zilizopita
Chapisha Maoni