Agathon Rwasa, mpinzani na mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi uliofanyika Burundi na rais Pierre Nkurunziza kuibuka mshindi ametoa wito wa kurejea kwa uchaguzi.
Rais Nkurunziza ametangazwa kuwa rais baada ya kuchaguliwa kwa asilimia 69.
Vyama vya upinzani vilisusia uchaguzi huo kwa madai kuwa rais Nkurunziza kuwania kiti cha urais katika muhula wa 3 ni kinyume ya katiba na mkataba wa Arusha.
Licha ya kuchukua nafasi ya pili, Rwasa alifahamisha
kutokutambua matokeo ya uchaguzi na kusema kuwa wazo la serikali ya
muungano ni jambo la kuungwa mkono iwapo malengo yake itakuwa ni kuandaa
uchaguzi wa haki na demokrasia.
CHANZO TRT SWAHILI
Sherehe za siku ya Kiswahili duniani zafana nchini Algeria
-
BALOZI wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, amesema lugha ya
Kiswahili inaendelea kukua na kuenea duniani ambapo sasa inazungumzwa na
watu ...
Saa 2 zilizopita
Chapisha Maoni